Wednesday, June 8, 2011

Serikali iko wapi?

Na Samson Kamalamo

JUMA lililopita, gazeti moja la kila siku, liliripoti kuhusu kukamatwa kwa raia wa Marekani, huko Tarime katika eneo la Nyamongo au North Mara.

Gazeti hilo liliendelea kubainisha kuwa Mmarekani huyo alikamatwa akipiga picha za matukio ya mgodi huo na kuzituma kwenda nchini kwao, haijulikani kwa matumizi gani.

Haikuelezwa kama Mmarekani huyo alikuwana kibali kutoka Idara ya Habari (MAELEZO) kumwezesha kupiga picha katika maeneo mbalimbali ya nchi tena akiwa pekee yake na kuzituma popote anapopenda.

Ninachofahamu, ni kwamba, wote wanaokuja nchi hii wakiwa waandishi wa habari au watu wengine lakini wakiwa na dhamira ya kupiga picha, wanapaswa kuwa na vibali maalum vya maeneo husika, na mara nyingi huambatana na maofisa husika, ili kuhakikisha picha zinazopigwa ni zile tu zilizoombewa kibali.

Katika hili, FIKRA PEVU haina budi kuuliza, Serikali iko wapi? Serikali inayozungumziwa hap si lazima iwe ile kuu, isipokuwa hata zile za vijiji. Ziko wapi, kiasi cha kuruhusu mgeni kufanya anachotaka katika ardhi ya nchi huru kama Tanzania?

Kitendo cha Mmarekani yule kukamatwa akifanya shughuli zake hizo hata kama ni kwa kofia ya kikundi au chama fulani, ni cha kihaini na hakipaswi kuvumbiwa macho na kuachiwa kimalizike hivi hivi tu.

Huu sasa ndiyo wakati wa kuonyesha hao wenye vikundi na washirika wawageni hao kwamba Serikali iko makini na kwamba itasimamia katika sheria na kanuni zilizopo.

Hakuna njia mbadala ya kuonyesha makucha hayo ya serikali isipokuwa kwa Mmarekani huyo na washirika wake wazalendo, wote kwa pamoja kufunguliwa mashitaka ya uhaini na kufikishwa mahakamani mapema iwezekanavyo.

Sidhani kama iko haja ya kuchelewesha jambo hilo, eti kwa visingizio vya kusubiri kukamilika kwa upepelezi. Ni upelelezi gani utatakiwa kufanyika ilhali mtuhumiwa kakutwa na ngozi?

Ngozi yake ni kamera na vifaa vingine vya mawasiliano alivyokutwa navyo eneo la tukio, vinavyomwezesha kuwasiliana na mahali popote pale ulimwenguni.

Mmarekani huyo na wengine wote walioshirikiana naye kwa misingi kwamba wanaweza kufanya lolote bila kufanywa chochote, lazima achukuliwe hatua za kisheria, hili iwe fundisho kwa wengine wanaodhani serikali imelala.

Tujiulize, ni wageni wangapi wamekuwa wakitumiwa na vikundi hivi kuchafua taswira ya Tanzania katika anga za kimataifa? Bila shaka wapo wengi, lakini kwa huyu, arobani yake imefika.

Kukakatwa kwa huyo Mmareni kunapaswa kutumiwa kama taarifa muhimu katika kubaini kwamba nchi yetu imekuwa ikiingiliwa na kuchafuliwa na watu wengi pasipo watanzania wenyewe kujua.

Hii ni dhahiri kwamba vikundi, mashirika yasiyo ya kiserikali, makampuni na hata vyama vya siasa, ama kwa kujua au kutokujua, vimekuwa vikiwezesha Tanzania kuzungumzwa vibaya huko nje na kuonekana kuwa ni taifa lisilostahili kuwepo.

Kuendelea kuvumilia vitendo vya namna hii pasipo kuvichukulia hatua kali ni sawa na kuwasaliti watanzania. Tufike mahali basi, siasa ikae pembeni na sheria ichukue mkondo wake.

Tukiendelea kuikumbatia siasa na kudhani kuruhusu kuwepo kwa maandamano kila kukicha kuwa ndiyo kuimarisha na kukuza demokrasi, huk ni kujidanganya. Ukweli tunajichimbia kaburi letu wenyewe.

Tufike mahali tupime. Na tufike mahali kubainishe wazi upi wakati wa siasa za nje yaani za majukwani na upi wakati wa siasa za ndani. Mbona huko demokrasia ilikopea hatuoni haya yanayotokea kwetu?

Fikra Pevu inaisii serikali iliyoko madarakani kuongeza uamkini kidogo na kusimamia katika sheria, hata kama kwa kufanya hivyo itaonekana kuwa inaminya demokrasia. Hiki kinachotokea sidhani kama ni demokrasia. Ni demokrasia ya wapi inayoruhusu mtu kugusa pua ya mwenzie?

Tuonane wiki ijayo. Wasalaa.

yl� o t H3 ��� 0pt;font-family:"Times New Roman","serif"'>

Hii ni dhahiri kwamba vikundi, mashirika yasiyo ya kiserikali, makampuni na hata vyama vya siasa, ama kwa kujua au kutokujua, vimekuwa vikiwezesha Tanzania kuzungumzwa vibaya huko nje na kuonekana kuwa ni taifa lisilostahili kuwepo.

Kuendelea kuvumilia vitendo vya namna hii pasipo kuvichukulia hatua kali ni sawa na kuwasaliti watanzania. Tufike mahali basi, siasa ikae pembeni na sheria ichukue mkondo wake.

Tukiendelea kuikumbatia siasa na kudhani kuruhusu kuwepo kwa maandamano kila kukicha kuwa ndiyo kuimarisha na kukuza demokrasi, huk ni kujidanganya. Ukweli tunajichimbia kaburi letu wenyewe.

Tufike mahali tupime. Na tufike mahali kubainishe wazi upi wakati wa siasa za nje yaani za majukwani na upi wakati wa siasa za ndani. Mbona huko demokrasia ilikopea hatuoni haya yanayotokea kwetu?

Fikra Pevu inaisii serikali iliyoko madarakani kuongeza uamkini kidogo na kusimamia katika sheria, hata kama kwa kufanya hivyo itaonekana kuwa inaminya demokrasia. Hiki kinachotokea sidhani kama ni demokrasia. Ni demokrasia ya wapi inayoruhusu mtu kugusa pua ya mwenzie?

No comments:

Post a Comment